Sheria za Shule
Kanuni za kiutu, kitaaluma, bweni na adhabu zinazotuongoza.

1. Sheria za kiutu
- Uwahi shuleni muda uliopangwa, uwepo muda wote wa masomo na wa kazi ukifuata ratiba ya shule.
- Uheshimu bendera, picha za viongozi na wimbo wa taifa unaotumiwa na shule.
- Uwe na tabia njema, heshima na utiifu kwa walimu, wafanyakazi, wanafunzi wenzako na majirani wa shule.
- Ukifikiwa au kukutana na mwalimu au mtu yeyote anayekuzidi umri usimame kumsalimia.
- Ukiitwa na mwalimu yeyote umuitikie mara.
- Uwe daima safi (mwili, nguo na vitu vyote unavyotumia).
- Uwe na nywele fupi; usifuge ndevu.
- Usijirembe kwa kutia nywele dawa, kujichora, kutia wanja n.k.
- Usiache kucha ndefu wala kupaka rangi au hina.
- Usivae kofia, jaketi, viatu vya ghorofa wala mapambo yoyote.
- Uvae daima sare ukiwa shuleni, kwa shughuli za kishule, hospitalini au safarini kwenda/kutoka shuleni.
- Usionekane katika mazingira ya wasiwasi wala kujihusisha na ulevi na uvutaji wa aina yoyote.
- Usiwe na urafiki wa kimapenzi.
- Darasani ukae mahali pako, pasipo kuhamahama wala kuchanganyikana na jinsia nyingine.
- Uthamini kazi za aina zote na kushirikiana na wenzako katika usafi na utunzaji wa mazingira.
- Ulinde mali yako binafsi na ya shule.
- Usitoe dawati nje ya jengo lake pasipo agizo au ruhusa.
- Ni marufuku kuiba, kugombana, kupigana, kutumia lugha chafu, kuchonganisha au kufanya mgomo.
- Usitembelee nyumba za walimu wala bweni la jinsia tofauti.
- Usitoroke shule; toa taarifa kama utashindwa kuhudhuria masomo.
- Usilete shuleni simu, redio n.k. la sivyo utafukuzwa mara moja.
- Ukubali mamlaka ya wanafunzi viongozi katika kushauri, kuonya na kuadhibu.
- Usikatae adhabu.
2. Sheria za kitaaluma
- Uwe msikivu na mtekelezaji wa maagizo na mashauri ya walimu.
- Ukamilishe kazi zote zinazotolewa kwa wakati unaotakiwa.
- Uwe mtulivu muda wote darasani, mwalimu awepo au asiwepo.
- Ushirikiane vema na walimu na wanafunzi wenzako.
- Ujitahidi kufanya vizuri mitihani ya mara kwa mara — kuepuka kuondolewa shuleni.
- Ni kosa kubwa kuibia, kusaidiwa au kusaidia katika mtihani wowote.
3. Sheria za nyongeza kwa wanaokaa bweni
- Uvae sare muda wote uwapo shuleni au bwenini, bila kuichanganya na vazi lingine.
- Ukienda darasani usirudi bwenini wakati wa vipindi bila ruhusa.
- Uzingatie muda wa chakula; huruhusiwi kukipeleka bwenini.
- Usiende nje bila ruhusa maalumu; ukienda kwenye ibada uvae sare na kurudi shuleni mara.
- Usimpokee mgeni yeyote tofauti na walioandikwa na mzazi, wala nje ya siku za kutembelewa.
- Usiwasiliane na mtu yeyote bila mkuu wa bweni kujua.
4. Adhabu
- Kukwepa au kuibia mtihani: utaandikiwa alama sifuri (0%).
- Makosa madogo: maonyo mawili yataandamana na adhabu shuleni na barua ya kukiri kosa.
- Makosa makubwa: kusimamishwa siku au wiki kadhaa, hadi kufukuzwa shule.
- Ukipoteza/kuharibu kitabu au kitu cha shule: utatakiwa kununua kipya au kupoteza fedha za tahadhari.
- Hutarudishiwa vitu visivyotakiwa shuleni vikinyang’anywa na uongozi.
